Mke wa mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William, amejifungua mtoto wa kiume. Kate Middleton, amejifungua mtoto huyo jana Jumatatu katika hospitali ya St. Mary's, iliyoko magharibi mwa London, akiwa na uzito wa kilo 3.79. Kate alishikwa na uchungu wa kujifungua mapema jana Jumatatu asubuhi na kupelekwa katika hospitali ya St. Mary's. Jinsia ya mtoto huyo haikujulikana kipindi chote cha ujauzito, kwa sababu Kate na William hawakutaka kujua jinsia ya mtoto wao, hadi pale atakapozaliwa. Kulingana na utamaduni wa Uingereza, taarifa rasmi za kuzaliwa kwa mtoto huyo, zilitolewa nje ya milango mikuu ya kasri la Buckingham, jana Jumatatu jioni.
aww ni furaha iliyoje kwan jina limeongezeka hapo usiku wa jana baba kwa sasa
Prince william akiwa amemshika mwanye dk chache mara baada ya kuzaliwa usiku wa jana majira ya 4:24pm.
huo ndio ujumbe ambao uliweka nje ya jumba hilo la kifalme mara baada ya kuzaliwa kwa mtoto huyo wa kiume.
kwa usiku wa Jana ndivyo jiji la London Uingereza lilivyokuwa kwani kulitawala rangi Nyekundu na Blue kuashiria furaha kwa ujio wa mtoto huyo wa kiume mjukuu wa Princess DIANA.
haaha kama kawa mambo ya kupiga mafoto na kushangaa
baadhi ya wananchi na wapenzi wa familia ya Princess DIANA wakiwa nje ya Jumba la Kiflalme baad ya kupata taarifa juu ya kuzaliwa kwa baby boy of Prince William and Catherine.
ndivyo ilikuwa siku ya jana jumatatu asubuhi hadi ulipoingia usiku alipozaliwa mtoto ambaye anategemewa kuja kuwa KING hapo baadae










No comments:
Post a Comment